- Jul 8, 2023
- 1,320
- 2,996
- 2,100
Biashara ya movies store au library ni biashara nzuri sana kama utaifanya kwa uweledi mzuri, ni biashara isiyotumia nguvu sana.
Kwa mtaji wa million 2 unaweza kufanya hii biashara ikakupatia kipato kizuri sana.
Kwa atakaye penda mchanganuo wa biashara hii nakukaribisha..
Mchanganuo

Kwa mtaji wa million 2 unaweza kufanya hii biashara ikakupatia kipato kizuri sana.
Kwa atakaye penda mchanganuo wa biashara hii nakukaribisha..
Mchanganuo


MCHANGANUO WA BIASHARA YA MOVIES STORE/LIBRARY...
KWA MTAJI WA MILLIONS 2 TUU.
@The great manenge..
kama nilivyosema hii biashara nzuri basi tuanze na vitu vya umuhimu..
A)=FREM/BANDA
Hapa unaweza kukodi frem au ukajenga banda lako la mbao tu.
FREMU kwa kila mwenzi utakodi kwanzia 50000-80000 ita range hapo,basi tu assume umekodi kwa 70000 ambapo kwa miezi 6 ni 420000
BANDA utalijenga la mbao mpaka kuisha utatumia 450000 lenye ukubwa wa 6 kwa 6(nina maanisha futi 6 urefu6,upana 6)..
Basi tukienda na fremu tutakodisha kwa 420000 kwa miezi 6 na tukienda na banda tutajenga kwa 450000 na tutamlipa mwenye eneo 1000 au 2000
Kwa siku.
Basi twende na FREMU..
B)=VIFAA VYA OFFICE
1) Computer
Hapa ndo penye umuhimu sana maana computer ikiwa mpya na yenye ubora ndio itakurahisishia kazi zako Fasta bila kuchosha wateja kusubiri kwa mda mrefu.
Aina za computer na zijua nyingi sana na zote nisha tumia. Ila computer niliyotokea kuiamini sana tena inaroho ngumu sana. FUJITSU MACHINE CHUMA CHA MJERUMANI HII COMPUTER NI HATARI SANA INAPIGA KAZI MFANO HAKUNA. Utanunua kwanzia core 3 mpaka core 7 bei ya sasa core 7 ni cpu mpya ni 350000..
Na monitor tutachukua ya dell ndizo nzuri huwa hazipati moto sana tutanunua kwa 120000 hapo ni kipya. Mpaka hapo tutakuwa tumetumia
Fremu=420000
Cpu =350000
Monitor=120000
Mpaka hapo tutakuwa tumetoa 890000 kwenye ile million yetu 2..
Hiyo machine ya fujitsu ina sata 4 za hard disk kuacha ya window na mlango wa CD. Basi tutanunua internal hardidisk ya Terabytes 4 tutachukua 4 kabisa. Terabytes 4 bei=120000 zikiwa 4=480000.
Mpaka hapo tutakuwa tumetumia
890000+480000=1370000. Kwenye ile million yetu 2. Mpaka hapo tutakuwa tumefanya yafuatayo.
1ffice
2:vifaa.
Tutakuwa tumebakiwa na 630000 kwenye ile 2millions.
Tutatoa laki 230000 hapo tutanunua kiti cha wateja kwa 80000 lile la sofa
,15000 kiti chako cha kukalia.
Inabaki 135000 kwenye ile 230000 .
Tutanunua used meza nzuri kwa 100000. Pia 35000 utampa mtu aandikie matangazo kwenye office huduma unayotoa.
Kule kwenye mzigo wetu wa million 2 tutakuwa tumebakiwa na 400000 tu
Mpaka hapo tutakuwa tumekamilisha office kwa asilimia 80%.
Sasa hapo hatuweki CD yeyote ukutani tutabandika poster kwenye kuta zote officine ambapo poster 1 ya A3 NI 1000
na ndogo za A4 ni 500 kwenye ile 4000000 tutatoa 50000 kwa ajili posters tu.
Sasa hiyo 350000 iliyobaki hapo ndo kwenye kazi kubwa iliyobaki.
**Toa 200000 nenda kwa mshikaji mwenye movies store bonga naye mwambie kila season moja ya movies atakupa kwa 500 sasa hapo chagua season zote kali zinazotamba utampa 150000 ile 50000 iliyobaki chagua single movies kali zinazotamba sasa.
**Mpaka hapo kwenye ule mzigo wetu wa 2 millions tutakuwa tumebakiwa na 150000 tuu,toa 70000 kanunua external hardisk (gb 500) kwa ajili ya kubebea movies ukienda kuchukua kila week.
Basi tutabakiwa na 80000 mpaka hapo,toa 50000 nenda kwa wanauza movies zilizotafsiriwa mwambie unaanza biashara ya library kwahiyo unahitaji mzigo wa season na single zilizotafsiriwa,hiyo ela kwao watakujazia hata terabytes 2.
Hapo tutakuwa tumekamilisha kila kitu cha officine yani office itakuwa imesimama vyema,imependeza kweli kweli..
**mpaka hapo kwenye ule mzigo wa 2 millions tumebakiwa na 20000 tuu.
Hiyo tunaiacha kwa dharura ..
MAMBO YA KUZINGATI TENA MUHIMU:..
1>-KAULI NZURI KWA WATEJA
2>-FANYA KAZI KWA USTADI MKUBWA
3>-KUWA UPDATE NA MOVIES
4>-WAFURAHISHE WATEJA
hii biashara inahitaji ujanja sana,kupata 35000-50000 kwa siku kawaida sana.
..............HITIMISHO............
Last edited by a moderator: